Vitu Muhimu vya Kufanya Baada ya Kujifungua
Posted by Afya4all Admin on May 5, 2022 in Ushauri na Mbinu
Omba cheti cha kuzaliwa cha mtoto sasaFanya kutengeneza cheti cha mwanao katika ofisi za RITA, mara
utakapokipata kihifadhi vizuri na tengeneza nakala mbili alafu hifadhi.
Ukiomba cheti mapema inapunguza usumbufu hapo baadae.
Omba likizo ya uzazi kama unafanya kazi
Mara baada ya kujifungua hakikisha unatoa taarifa katika uongozi wa
kazini kwako ili upate haki zako kama mama mzazi ikiwemo likizo.
Tuma taarifa ya kujifungua kwako kwa ndugu,jamaa na mrafiki
Sambaza habari njema kwa watu! Kwa marafiki, ndugu na majirani.
Andika salamu za shukurani
Kama una bahati ya kubarikiwa na marafiki wengi na familia
waliokujali tangu awali na kumtunuku mtoto na wewe zawadi, kumbuka
kuwashukuru, ni ishara ambayo haisauliki.
Anza kujipendezesha
Anza kujipendezesha mapema ili utakaporudia maisha yako usipate shida.
Jaribu kumlaza tumboni
Anza kumlaza mtoto juu ya kifua chako na jaribu kumnyanyua kichwa
chake ili akuangalie, hii itasaidia kukaza misuli ya shingo na mgongo.
Nunua nguo za uzazi
Nunua nguo kama madera, gauni kubwa zitakazokupa uhuru wakati wa
kunyonyesha, sidiria za kunyonyeshea ni muhimu na chupi kubwa
zisizobana.
Anza mazoezi
Si rahisi kurudia utaratibu wa mazoezi mara baada ya kujifungua,
lakini kutembea kunasiadia kuinua hisia zako na mwili kurejea hali ya
awali.
Kula sawa
Kula matunda mengi na mbogamboga, nafaka kama ngano, wali,shayiri,
mahindi. Nafaka ambazo hazijakobolewa ni nzuri. Maziwa na bidhaa zake na
protini inayotoka kwenye samaki,karanga,maharage. Epuka vyakula vya
mafuta hasa kwenye mifugo.
Kunywa maji mengi
Bado kuna mengi yanayoendelea kwenye mwili wako baada ya
kujifungua,kwahiyo kunywa maji mengi kutasaidia kuweka mambo sawa.
Tafuta kopo zuri la maji na tembea nalo kila mahali.
Ongeza mahitaji ya mtoto
Licha ya maandaklizi ya mtoto,kuna baadhi ya vitu vinahitajika
kuongezwa kama nepi au diaper na jaribu kuziweka karibu mfano
bafuni,kwenye begi la mtoto, sebuleni na hata chumbani kwa mtoto.
Toka nje mara moja kwa siku
Hata kama ni kuzunguka nyuma ya nyumba, pata hewa safi itakusaidia kuondoa uchovu na mawazo.
Pata msaada kama unahitaji
Kama umechoka ongea na daktari wako. Pata msaada, ongea na mshauri
nasaa au pata matibabu ya msongo wa mawazo baada ya kujifungua,sio jambo
la kuona aibu. Matatizo ya hisia baada ya kujifungua yanaletwa na
mabadiliko ya homoni na haina maana wewe ni mvivu, kichaa au mama mbaya.
Mjue mwanao
Hili ni jambo la muhimu sana-jaribu kufurahia muda na mwanao mchanga.
Ni jambo la kuchosha,kukasirisha, kuchanganya na kuleta changamoto,
lakini ni jambo la muhimu sana. Sio kila mtu anafurahia kila mda lakini
jitahidi kutafuta kitu kizuri kila siku.
Fanya kutengeneza cheti cha mwanao katika ofisi za RITA, mara utakapokipata kihifadhi vizuri na tengeneza nakala mbili alafu hifadhi. Ukiomba cheti mapema inapunguza usumbufu hapo baadae.
Mara baada ya kujifungua hakikisha unatoa taarifa katika uongozi wa kazini kwako ili upate haki zako kama mama mzazi ikiwemo likizo.
Sambaza habari njema kwa watu! Kwa marafiki, ndugu na majirani.
Kama una bahati ya kubarikiwa na marafiki wengi na familia waliokujali tangu awali na kumtunuku mtoto na wewe zawadi, kumbuka kuwashukuru, ni ishara ambayo haisauliki.
Anza kujipendezesha mapema ili utakaporudia maisha yako usipate shida.
Anza kumlaza mtoto juu ya kifua chako na jaribu kumnyanyua kichwa chake ili akuangalie, hii itasaidia kukaza misuli ya shingo na mgongo.
Nunua nguo kama madera, gauni kubwa zitakazokupa uhuru wakati wa kunyonyesha, sidiria za kunyonyeshea ni muhimu na chupi kubwa zisizobana.
Si rahisi kurudia utaratibu wa mazoezi mara baada ya kujifungua, lakini kutembea kunasiadia kuinua hisia zako na mwili kurejea hali ya awali.
Kula matunda mengi na mbogamboga, nafaka kama ngano, wali,shayiri, mahindi. Nafaka ambazo hazijakobolewa ni nzuri. Maziwa na bidhaa zake na protini inayotoka kwenye samaki,karanga,maharage. Epuka vyakula vya mafuta hasa kwenye mifugo.
Bado kuna mengi yanayoendelea kwenye mwili wako baada ya kujifungua,kwahiyo kunywa maji mengi kutasaidia kuweka mambo sawa. Tafuta kopo zuri la maji na tembea nalo kila mahali.
Licha ya maandaklizi ya mtoto,kuna baadhi ya vitu vinahitajika kuongezwa kama nepi au diaper na jaribu kuziweka karibu mfano bafuni,kwenye begi la mtoto, sebuleni na hata chumbani kwa mtoto.
Hata kama ni kuzunguka nyuma ya nyumba, pata hewa safi itakusaidia kuondoa uchovu na mawazo.
Kama umechoka ongea na daktari wako. Pata msaada, ongea na mshauri nasaa au pata matibabu ya msongo wa mawazo baada ya kujifungua,sio jambo la kuona aibu. Matatizo ya hisia baada ya kujifungua yanaletwa na mabadiliko ya homoni na haina maana wewe ni mvivu, kichaa au mama mbaya.
Hili ni jambo la muhimu sana-jaribu kufurahia muda na mwanao mchanga. Ni jambo la kuchosha,kukasirisha, kuchanganya na kuleta changamoto, lakini ni jambo la muhimu sana. Sio kila mtu anafurahia kila mda lakini jitahidi kutafuta kitu kizuri kila siku.